Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 9:5
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Solomono alisimama kwenye mazabahu ya Yawe, mbele ya Waisraeli wote, aliinua mikono yake juu,


tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,


Solomono alipomaliza kusema maombi hayo yote na ombi lake kwa Yawe, alisimama kutoka pale mbele ya mazabahu ya Yawe, pahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu.


Solomono alikuwa ametengeneza mimbari ya shaba ambayo aliweka katikati ya kiwanja. Urefu na upana wake ulikuwa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili na tano. Akapanda juu ya mimbari na kupiga magoti mbele ya watu wote wa Israeli, akainua mikono yake kuelekea mbinguni.


Niliposikia hayo nikaikaa chini na kulia, nikaomboleza kwa siku za kutosha. Nikafunga kula na kumwomba Mungu wa mbinguni,


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Musa akamwambia: “Mara tu nitakapotoka inje ya muji nitainua mikono na kumwomba Yawe. Ngurumo itakoma na hakutakuwa mvua ya mawe tena kusudi utambue kwamba dunia ni ya Yawe.


Basi, Musa akaondoka katika nyumba ya mufalme, akatoka inje ya muji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Yawe. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua ikaacha kunyesha katika dunia.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Wakati huo, mimi Danieli, nilikuwa nikiomboleza kwa muda wa majuma matatu.


Kisha akajitenga nao na kuenda kwenye hatua ya mutu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba akisema:


Lakini muda ule ulipotimia tukaondoka na kuendelea na safari yetu. Waamini wote pamoja na wanawake na watoto wao wakatusindikiza mpaka mbali na hata kufika kwenye kivuko cha muji. Kule sisi wote tukapiga magoti na kuomba.


Kwa sababu hiyo ninapiga magoti mbele ya Baba Mungu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ