Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 9:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Tutavunja amri zako tena na kuoana na watu hawa wanaotenda maovu haya? Hautatukasirikia na kutuangamiza kabisa, na kusibaki hata mumoja wetu muzima wala yeyote wa kutoroka?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 9:14
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuhani Ezra akasimama kwa kuzungumuza na watu, akawaambia: “Hamukukuwa waaminifu kwa kuoa wanawake wa kigeni, na hivyo mumeiongezea Israeli kosa.


Wayuda wanaoa wanawake wa kigeni na kuwaoea wana wao vilevile. Hivyo, taifa takatifu la Mungu limechanganyika na watu wa mataifa mengine. Vilevile wasimamizi na wakubwa ndio wa kwanza kutenda maovu hayo.”


Lakini sasa, ee Yawe, Mungu wetu, kwa muda mufupi umetuonyesha huruma yako na kuwawezesha wamoja kati yetu kuponyoka kutoka katika utumwa na kuishi kwa usalama pahali pako patakatifu. Pahali pa utumwa, umetupa furaha na maisha mapya.


Babu zetu hawakufanya uovu wa namna hiihii na kumusukuma Mungu wetu kutuletea hasara pamoja na muji huu? Na munazidi kuamusha kasirani yake juu ya watu wa Israeli kwa kuchafua siku ya Sabato.”


Musifanye agano lolote nao, wala na miungu yao.


Sasa, usijaribu kunizuia. Uniache niwaangamize kwa kasirani kali. Kisha kutokana nawe nitaunda taifa kubwa.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Mumesahau uovu wa babu zenu, uovu wa wafalme wa Yuda, uovu wa wake wao na uovu wenu ninyi wenyewe na wa wake wenu, ambao muliufanya katika inchi ya Yuda na kwenye barabara za Yerusalema?


Usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo nimekutawanya kati yao, lakini wewe sitakuangamiza. Nitakuazibu kadiri unavyostahili, sitakuacha bila kukuazibu.


Hata hivyo, nitawaacha wengine wabaki wazima; wamoja kati yenu wataponyoka upanga nao watasambazwa katika inchi mbalimbali.


Mujitenge na watu hawa, niwaangamize sasa hivi.


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Basi sasa tuseme nini? Tuendelee kuishi katika zambi kusudi neema ya Mungu izidi kuongezeka?


Uniache niwaangamize, nifute jina lao toka katika dunia. Nami nitakufanya wewe kuwa taifa lenye nguvu na kubwa kuliko wao.’


Hata huko kwenye mulima Horebu, mulimukasirikisha Yawe, naye alikasirika sana, kiasi cha kutaka kuwaangamiza.


Na kwa upande wenu niliwaamuru musifanye agano na wenyeji wa inchi hii na kwamba mazabahu zao mutazibomoa. Lakini ninyi hamukuitii amri yangu. Kwa nini mambo haya?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ