naye akamwambia: “Kwa sababu umetoa ombi hili, na haukujiombea maisha marefu au mali, na wala haukuomba waadui zako waangamizwe, lakini umejiombea hekima ya kutoa hukumu au kutenda haki,
Kura ya kuchagua wa kulinda mulango wa upande wa mashariki ikamwangukia Selemia. Wakapiga kura vilevile kwa ajili ya mwana wake Zekaria, aliyekuwa mushauri mwenye hekima, ikamwangukia kura ya mulango wa upande wa kaskazini.
Nikawakusanya pamoja watu wote pembeni ya muto unaoelekea muji wa Ahava. Kule, tukapiga kambi kwa muda wa siku tatu. Nikaangalia kati ya watu wote pamoja na makuhani, lakini sikupata Walawi kati yao.
Nikawatuma kwa Ido, kiongozi wa jamii ya watu kule Kasifia, nikimwomba yeye pamoja na wenzake watumishi wa nyumba ya Mungu, watuletee watu watakaotumika katika nyumba ya Mungu.
Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.