Ezra 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021-14 Hayo ndiyo majina ya viongozi wa ukoo za watu waliorudi pamoja nami Ezra kutoka Babeli, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta: Gersomi, wa ukoo wa Finehasi; Danieli, wa ukoo wa Itamari; Hatusi, wa ukoo wa Daudi; mwana mumoja wa ukoo wa Sekania; Zakaria, wa ukoo wa Parosi, pamoja na wanaume mia moja na makumi tano wa ukoo wake, walioandikishwa pamoja; Eliyoenayi mwana wa Zerahia, wa ukoo wa Pahati-Moabu, pamoja na wanaume mia mbili; Sekania mwana wa Yahasieli, wa ukoo wa Zatu, pamoja na wanaume mia tatu; Ebedi mwana wa Yonatani, wa ukoo wa Adini, pamoja na wanaume makumi tano; Yesaya mwana wa Atalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume makumi saba; Zebadia mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Sefatia, pamoja na wanaume makumi nane; Obadia mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume mia mbili kumi na wanane; Selemoti mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume mia moja na makumi sita; Zakaria mwana wa Bebayi, wa ukoo wa Bebayi, pamoja na wanaume makumi mbili na wanane; Yohanani mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu mia moja na kumi; Elifeleti, Yueli na Semaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume makumi sita, (hawa walirudi kisha); Utayi na Zakuri, wa ukoo wa Bigwayi pamoja na wanaume makumi sita. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |