Kwa wema wa Mungu, nimepata musaada wa mufalme na wakubwa wake wenye uwezo mukubwa. Nilipata nguvu kwa sababu Yawe, Mungu wangu, alikuwa pamoja nami, hata nikawakusanya viongozi wa Israeli kusudi warudi pamoja nami.”
Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.
Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.
Katika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza, tukasafiri kutokea kwenye muto Ahava, kwenda Yerusalema. Mungu wetu alikuwa pamoja nasi, akatulinda na waadui na washambulizi katika njia.
Nikawaelezea jinsi Mungu alivyokuwa pamoja nami akinitendea kwa wema wake. Nikawaelezea vilevile maneno ambayo mufalme alikuwa ameniambia. Wao waliposikia hayo, wakasema: “Sasa, na tuanze kazi ya ujenzi.” Hivyo wakajitayarisha kwa kazi hiyo njema.
Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.
Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.