Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Artasasta, Ezra akafunga safari kutoka Babeli kwenda Yerusalema. Alikwenda pamoja na watu wamoja wa Israeli, makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa milango na watumishi wa hekalu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:7
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Viongozi wa Wayuda waliendelea vizuri sana na kazi ya ujenzi wa hekalu, wakitiwa moyo na nabii Hagai na Zakaria mwana wa Ido. Wakamaliza ujenzi wa hekalu kama walivyoamriwa na Mungu wa Israeli, na kama walivyoagizwa na mufalme Kiro, mufalme Dario na mufalme Artasasta, wa Persia.


Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.


Wakafika Yerusalema katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Artasasta.


Hili ni simulizi la Nehemia mwana wa Hakalia. Ilitukia kwamba, nilipokuwa katika muji mukubwa wa Susani, katika mwezi wa Kisileu wa mwaka wa makumi mbili,


Haya ndiyo majina ya makuhani na Walawi waliorudi toka katika uhamisho pamoja na Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Kuhani Mukubwa Yesua. Makuhani walikuwa: Seraya, Yeremia, Ezra, Amaria, Maluku, Hatusi, Sekania, Rehumu, Meremoti, Ido, Ginetoni, Abiya, Miyamini, Madia, Bilga, Semaya, Yoyaribu, Yedaya, Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hao walikuwa ni wakubwa wa makuhani na wandugu zao wakati wa Yesua.


Katika mwezi wa Nisani, kwa mwaka wa makumi mbili wa utawala wa mufalme Artasasta, wakati divai ilipokuwa mbele yake, nilitwaa divai na kumupatia mufalme. Mpaka sasa nilikuwa sijapata kuwa na huzuni mbele yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ