Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:6
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Lakini Mungu alikuwa anawalinda viongozi wa Wayuda, kwa hiyo wakubwa hao hawakuwakataza mpaka pale walipomwandikia mufalme Dario na kupata maoni yake.


Kwa muda wa siku saba watu walisherehekea kwa furaha sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa sababu Yawe aliwajalia furaha na kumupa mufalme wa Asuria moyo wa upendo kwao, akawasaidia katika kazi za ujenzi wa nyumba ya Mungu, wa Israeli.


Mimi mufalme Artasasta, ninatoa amri kwa walinzi wa hazina wote katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kwamba kitu chochote Ezra atakachohitaji, kuhani na mwandishi wa Sheria ya Mungu wa mbinguni, mutamupa, tena bila kusita,


Kwa wema wa Mungu, nimepata musaada wa mufalme na wakubwa wake wenye uwezo mukubwa. Nilipata nguvu kwa sababu Yawe, Mungu wangu, alikuwa pamoja nami, hata nikawakusanya viongozi wa Israeli kusudi warudi pamoja nami.”


mwana wa Abisua mwana wa Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni, Kuhani Mukubwa.


Yawe akaifanikisha sana safari yao waliyokuwa wameianza siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.


Hayo ndiyo majina ya viongozi wa ukoo za watu waliorudi pamoja nami Ezra kutoka Babeli, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta: Gersomi, wa ukoo wa Finehasi; Danieli, wa ukoo wa Itamari; Hatusi, wa ukoo wa Daudi; mwana mumoja wa ukoo wa Sekania; Zakaria, wa ukoo wa Parosi, pamoja na wanaume mia moja na makumi tano wa ukoo wake, walioandikishwa pamoja; Eliyoenayi mwana wa Zerahia, wa ukoo wa Pahati-Moabu, pamoja na wanaume mia mbili; Sekania mwana wa Yahasieli, wa ukoo wa Zatu, pamoja na wanaume mia tatu; Ebedi mwana wa Yonatani, wa ukoo wa Adini, pamoja na wanaume makumi tano; Yesaya mwana wa Atalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume makumi saba; Zebadia mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Sefatia, pamoja na wanaume makumi nane; Obadia mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume mia mbili kumi na wanane; Selemoti mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume mia moja na makumi sita; Zakaria mwana wa Bebayi, wa ukoo wa Bebayi, pamoja na wanaume makumi mbili na wanane; Yohanani mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu mia moja na kumi; Elifeleti, Yueli na Semaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume makumi sita, (hawa walirudi kisha); Utayi na Zakuri, wa ukoo wa Bigwayi pamoja na wanaume makumi sita.


Kwa neema ya Mungu, wakatuletea Serebia, mutu mwenye akili na Mulawi wa ukoo wa Mali, pamoja na wana wake na wandugu zake kumi na wanane.


Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.


Katika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza, tukasafiri kutokea kwenye muto Ahava, kwenda Yerusalema. Mungu wetu alikuwa pamoja nasi, akatulinda na waadui na washambulizi katika njia.


Watu hao waliishi wakati wa Yoyakimu mwana wa Yesua mujukuu wa Yosadaki na vilevile wakati wa Nehemia aliyekuwa liwali wa jimbo; na hata wakati wa Ezra kuhani na mwandishi.


Ndugu zake hawa waliimba kwa ala za muziki za mufalme Daudi, mutu wa Mungu, ni kusema Semaya, Azareli, Milalayi, Gilalayi, Maayi, Netaneli, Yuda na Hanani, wakatanguliwa na Ezra mwandishi.


Kisha nikaondoka usiku, mimi pamoja na watu wachache; sikumwambia mutu yeyote yale ambayo Mungu alikuwa ameyaweka ndani ya moyo wangu kwa ajili ya Yerusalema. Lakini siku moja usiku, nikaondoka na kutwaa watu wachache tu. Sikupeleka nyama yeyote isipokuwa punda niliyepanda juu yake mimi mwenyewe.


Nikawaelezea jinsi Mungu alivyokuwa pamoja nami akinitendea kwa wema wake. Nikawaelezea vilevile maneno ambayo mufalme alikuwa ameniambia. Wao waliposikia hayo, wakasema: “Sasa, na tuanze kazi ya ujenzi.” Hivyo wakajitayarisha kwa kazi hiyo njema.


Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.


Hivyo, tukaendelea kufanya kazi yetu na nusu ya watu wakishika silaha tangu mapambazuko mpaka nyota zinapoonekana mbinguni.


Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Kesho yake, wakubwa wa ukoo pamoja na makuhani na Walawi wakakusanyika kwa Ezra mwandishi, kwa kujifunza Sheria.


Ezra, mwandishi, alikuwa akisimama kwenye mimbari ya mbao iliyotengenezwa kwa kusudi lile; na kwenye mukono wake wa kuume watu hawa walikuwa wakisimama: Matitia, Sema, Anaya, Uria, Hilkia na Masea; na kwenye mukono wake wa kushoto kulikuwa kunasimama watu hawa: Pedaya, Misaeli, Malkiya, Hasumu, Hasubadana, Zakaria na Mesulamu.


Watu waliposikia Sheria, wakaguswa ndani ya mioyo yao, halafu wote wakaanza kulia. Hivyo Nehemia aliyekuwa mutawala na Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliofundisha watu wakawaambia watu wote: “Siku hii ni siku takatifu kwa Yawe, Mungu wenu, hivyo musiomboleze wala kulia.


Kule kwa mulima Sinai ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao. Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli, masharti mazuri na amri.


Uwaonyeshe watu kuwa wewe ndiwe uliyetenda hayo. Wewe, ee Yawe, ndiwe uliyefanya hivyo.


Anatoa ujumbe wake kwa wazao wa Yakobo, nayo masharti na maagizo yake kwa Waisraeli.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo: “Mayungiyungi.” Mashairi ya Wakora. Wimbo wa mapenzi.


Mukono wako umukinge huyo uliyemurehemu; huyo uliyemuchagua kwa ajili yako.


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Musifikiri kwamba mukono wa Mungu ni mufupi, hata asiweze kuwaokoa, au kwamba masikio yake yamefungana, hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Ninyi munajidai kwamba muko na hekima, nanyi munafuata amri zangu mimi Yawe. Lakini kalamu ya uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”


“Walimu wa Sheria na Wafarisayo wamepewa madaraka ya kueleza Sheria ya Musa.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!


Wandugu zangu, sasa ninataka kuwakumbusha Habari Njema niliyowatangazia, ile muliyopokea na kuishika imara.


“Kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, na kushika kwa uangalifu amri ambazo ninawaamuru leo, yeye atawaweka juu ya mataifa yote katika dunia.


“Muangalie! Nimewafundisha masharti na maagizo kama vile Yawe, Mungu wangu alivyoniamuru nifanye, kusudi muyashike katika inchi munayokwenda kuirizi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ