Ezra 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20026 Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Hayo ndiyo majina ya viongozi wa ukoo za watu waliorudi pamoja nami Ezra kutoka Babeli, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta: Gersomi, wa ukoo wa Finehasi; Danieli, wa ukoo wa Itamari; Hatusi, wa ukoo wa Daudi; mwana mumoja wa ukoo wa Sekania; Zakaria, wa ukoo wa Parosi, pamoja na wanaume mia moja na makumi tano wa ukoo wake, walioandikishwa pamoja; Eliyoenayi mwana wa Zerahia, wa ukoo wa Pahati-Moabu, pamoja na wanaume mia mbili; Sekania mwana wa Yahasieli, wa ukoo wa Zatu, pamoja na wanaume mia tatu; Ebedi mwana wa Yonatani, wa ukoo wa Adini, pamoja na wanaume makumi tano; Yesaya mwana wa Atalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume makumi saba; Zebadia mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Sefatia, pamoja na wanaume makumi nane; Obadia mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume mia mbili kumi na wanane; Selemoti mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume mia moja na makumi sita; Zakaria mwana wa Bebayi, wa ukoo wa Bebayi, pamoja na wanaume makumi mbili na wanane; Yohanani mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu mia moja na kumi; Elifeleti, Yueli na Semaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume makumi sita, (hawa walirudi kisha); Utayi na Zakuri, wa ukoo wa Bigwayi pamoja na wanaume makumi sita.
Ezra, mwandishi, alikuwa akisimama kwenye mimbari ya mbao iliyotengenezwa kwa kusudi lile; na kwenye mukono wake wa kuume watu hawa walikuwa wakisimama: Matitia, Sema, Anaya, Uria, Hilkia na Masea; na kwenye mukono wake wa kushoto kulikuwa kunasimama watu hawa: Pedaya, Misaeli, Malkiya, Hasumu, Hasubadana, Zakaria na Mesulamu.