Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Ezra akasema: “Asifiwe Yawe, Mungu wa babu zetu, ambaye amemupatia mufalme moyo wa kupamba nyumba ya Yawe inayokuwa Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:27
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Hezekia na wakubwa wake walipokuja kuangalia mafungu yale, wakamushukuru Yawe na watu wake wa Israeli.


Kwa muda wa siku saba watu walisherehekea kwa furaha sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa sababu Yawe aliwajalia furaha na kumupa mufalme wa Asuria moyo wa upendo kwao, akawasaidia katika kazi za ujenzi wa nyumba ya Mungu, wa Israeli.


Kisha nikaondoka usiku, mimi pamoja na watu wachache; sikumwambia mutu yeyote yale ambayo Mungu alikuwa ameyaweka ndani ya moyo wangu kwa ajili ya Yerusalema. Lakini siku moja usiku, nikaondoka na kutwaa watu wachache tu. Sikupeleka nyama yeyote isipokuwa punda niliyepanda juu yake mimi mwenyewe.


Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.


Mungu akanipa moyo kuwakusanya viongozi na watu kwa kujua ukoo zao. Nikapata kitabu cha ukoo za watu waliorudi toka katika uhamisho mara ya kwanza, na hawa ndio waliokuwa wameandikwa ndani yake.


Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Vyura wakakufa katika nyumba, viwanja na kwenye baraza za nyumba na katika mashamba.


Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.


Utaletewa utukufu wa pori ya Lebanoni: mbao za shindano, mivinje na misunobari, zitumike kwa kupamba kiwanja cha hekalu langu; nami nitaleta utukufu hapo ninapokaa.


Yeye anapenda taifa letu na ni yeye aliyetujengea nyumba yetu ya kuabudia.”


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Nilipata furaha kubwa katika kuungana na Bwana kwa kuona munakumbuka tena kunisaidia. Sitaki kusema kwamba mulinisahau, lakini hamukupata wakati wa kuonyesha kwamba munanishugulikia.


“Hili ndilo agano nitakalofanya nao nyuma ya siku zile. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri, nikiziandika ndani ya mioyo yao.”


Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli katika siku zile: nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao, nikiziandika ndani ya mioyo yao. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ