Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.
Ninaamuru vilevile kwamba mutu yeyote ambaye hatatii amri hii, muti mumoja uongolewe kutoka katika nyumba yake na atundikwe juu yake. Tena, nyumba yake ifanywe kuwa yalala.
Mungu aliyeuchagua Yerusalema kuwa pahali pake pa kuabudiwa amwangushe mufalme au taifa lolote litakalopinga amri hii au kutaka kuiharibu nyumba hii ya Mungu inayokuwa katika Yerusalema. Ni mimi Dario niliyetoa amri hii na inapaswa kushikwa.