Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Utatwaa vilevile feza na zahabu yote utakayokusanya katika jimbo lote la Babeli, pamoja na matoleo ya mapenzi Waisraeli na makuhani wao waliyotoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wao inayokuwa Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:16
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Basi wakubwa wa ukoo, viongozi wa makabila ya Israeli, majemadari wa maelfu na wa mamia; vilevile na wakubwa wasimamizi wa kazi za mufalme walipotoa kwa mapenzi yao,


Halafu watu wakafurahi kwa sababu walitoa kwa mapenzi yao, maana kwa moyo wao wote walimutolea Yawe kwa mapenzi yao, naye mufalme Daudi akafurahi sana.


Kore mwana wa Imuna, Mulawi, aliyekuwa mulinzi wa Mulango wa Mashariki wa hekalu, akasimamia matoleo yote ya mapenzi kwa Mungu; na kugawanya matoleo kwa ajili ya Yawe na sadaka zinazokuwa takatifu kabisa.


Hakika nimekujengea nyumba tukufu kuwa makao yako ya milele.”


‘Tangu nilipowaondoa watu wangu kutoka inchi ya Misri, sikuchagua muji wowote katika makabila ya Waisraeli kusudi nijengewe nyumba nitakamoabudiwa; na sikumuchagua mutu yeyote akuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.


Lakini kisha nilichagua muji wa Yerusalema ukuwe muji ambamo nitaabudiwa, na nilimuchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’


Kila mumoja aliyebaki muzima katika uhamisho akitaka kurudi, wajirani zake wamusaidie kwa kumupa feza, zahabu, mali na nyama, pamoja na matoleo ya mapenzi yake kwa ajili ya nyumba ya Mungu kule Yerusalema.


Wajirani waliwasaidia watu hao kwa kuwapa vyombo vya feza, zahabu, mali, nyama na vitu vingine vya bei kali, mbali na vile vilivyotolewa kwa mapenzi.


Atukuzwe Yawe katika Sayuni, atukuzwe katika makao yake Yerusalema. Haleluia!


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ