Ezra 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Ninaamuru kwamba katika utawala wangu, Mwisraeli yeyote, au kuhani wao, au Mulawi, akitaka kurudi Yerusalema kwa mapenzi yake, anaweza kwenda pamoja nawe.
Kwa hiyo wakaamua kutoa tangazo katika inchi yote ya Israeli, kutoka Beri-Seba mpaka Dani, kwamba watu wakuje Yerusalema kwa kufanya sikukuu ya Pasaka ya Yawe, Mungu wa Israeli. Ilikuwa imepita muda murefu mbele ya watu kufanya Pasaka kulingana na sheria zake.
Basi sasa, kila mutu kati yenu ninyi wote munaokuwa watu wake, Mungu wake akuwe naye na aende katika Yerusalema huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yawe, Mungu wa Israeli, Mungu anayeabudiwa kule Yerusalema.
Kwa amri ya mufalme, tangazo hili lilitolewa katika muji mukubwa wa Susani, nao wajumbe wakalitangaza katika majimbo yote. Mufalme na Hamani wakaikaa chini kwa kunywa wakati watu katika muji wa Susani wanafazaika.
Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.