Beni-Hadadi mufalme wa Aramu alikusanya waaskari wake wote. Aliungwa mukono na wafalme wengine makumi tatu na wawili pamoja na farasi na magari yao ya vita. Aliuendea muji wa Samaria akauzunguka na kuushambulia.
Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.
Kisha mufalme akatuma jibu hili: Kwa mutawala Rehumu, kwa Simusayi, karani wa jimbo, pamoja na wenzenu wote wanaoishi Samaria na pahali pengine katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.
Nyuma ya mambo yale, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta wa Persia, kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Ezra. Ezra alikuwa mwana wa Seraya mwana wa Azaria mwana wa Hilkia
Huu ndio mufano wa barua ambayo Artasasta alimupa Ezra, kuhani na mwandishi, na mwenye ujuzi katika amri na masharti ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.
Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia.
Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.
Kutokea kwake kutafanywa na Mungu kwa wakati aliopanga. Yule ndiye Mungu anayestahili kutukuzwa, anayekuwa peke yake mutawala, mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.
Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”