Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza Sheria ya Yawe, kuitii na kuwafundisha watu wa Israeli masharti na maagizo zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:10
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, babu zetu, ulinde mupango wa namna hiyo na mafikiri ya namna hiyo ndani ya mioyo ya watu wako, na uelekeze mioyo ya watu wako kwako.


Rehoboamu alitenda maovu, kwa maana hakutayarisha moyo wake kwa kumutafuta Yawe.


Lakini, kuna wema fulani ndani yako. Umekwisha kuondoa sanamu zote za Ashera, mungu wa kike, na umejikaza sana kumutafuta Mungu kwa moyo wote.”


Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,


Huu ndio mufano wa barua ambayo Artasasta alimupa Ezra, kuhani na mwandishi, na mwenye ujuzi katika amri na masharti ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Nawe Ezra, kwa kutumia hekima Mungu wako aliyokupa, hiyo unayokuwa nayo, chagua wanasheria, na waamuzi watakaowaongoza wakaaji wote wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati ambao wanaishi kufuatana na Sheria ya Mungu wako. Na yule ambaye haijui Sheria hiyo, umufundishe.


Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.


Yobu, ukifanya moyo wako mukamilifu, utainua mikono yako kwa kumwomba Mungu!


lakini anafurahia sheria ya Yawe, na kuifikiri muchana na usiku.


Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.


Nimekusudia kwa moyo wote kufuata masharti yako milele.


Nitaishi katika uhuru kamili, maana ninashugulika na kanuni zako.


Linatokea kwa upande mumoja, na kuzunguka mpaka upande mwingine; hakuna kinachoweza kuepuka joto lake.


Waadui wamenitegea wavu waninase, nami ninaugua kwa huzuni. Wamenichimbia shimo katika njia yangu, lakini wao wenyewe wametumbukia humo.


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Ni kwa hiyo mutu yeyote atakayevunja hata amri moja inayokuwa ndogo kuliko zingine zote, na kuwafundisha watu wengine kufanya kama yeye, huyu atahesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni. Lakini yule atakayezishika na kuzifundisha wengine, huyu atahesabiwa kuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.


“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Katika kitabu changu cha kwanza nilikuelezea mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu alipoanza kazi yake


Mukumbuke kwamba mulikuwa watumwa kule Misri na mukuwe waangalifu kufuata masharti haya.


Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako; watafundisha watu wa Israeli sheria yako. Walawi watafukiza ubani mbele yako, sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Lakini kwa ngambo yako, ufundishe maneno yale yanayolingana na mafundisho ya kweli.


Haya ndiyo maneno unayopaswa kufundisha, ukiwaonya watu na kuwakaripia kwa mamlaka yote. Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Samweli akawaambia Waisraeli: “Kama munamurudilia Yawe kwa moyo wenu wote, basi mutupilie mbali miungu ya kigeni na sanamu za Astaroti. Muelekeze mioyo yenu kwa Yawe, na kumutumikia yeye peke yake; naye atawaokoa kutoka katika mikono ya Wafilistini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ