Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya mambo yale, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta wa Persia, kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Ezra. Ezra alikuwa mwana wa Seraya mwana wa Azaria mwana wa Hilkia

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 7:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Kwenda kwa Kuhani Mukubwa Hilkia kusudi ahesabu feza zilizoletwa katika nyumba ya Yawe, ambazo walinzi wa mulango walizikusanya kutoka kwa watu;


Kisha Kuhani Mukubwa Hilkia akamwambia Safanu, mwandishi: “Nimekipata kitabu cha Sheria katika nyumba ya Yawe.” Halafu Hilkia akamupatia Safanu kitabu, naye akakisoma.


Kisha Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme akamupeleka Seraya, Kuhani Mukubwa, kuwa mufungwa pamoja na Zefania, kuhani wa pili, na wakubwa wa walinda milango watatu.


Azariya mwana wa Hilkia mwana wa Mesulamu mwana wa Zadoki, mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu, aliyekuwa mukubwa wa nyumba ya Mungu;


Kisha Hilkia akamwambia Safani mwandishi: “Nimepata kitabu cha Sheria katika nyumba ya Yawe.” Halafu Hilkia akamupatia Safani kitabu kile.


Wakamwendea Hilkia, Kuhani Mukubwa, wakamupa feza zilizokuwa zimeletwa katika nyumba ya Mungu ambazo zilikusanywa na Walawi walinzi wa mulango, kutoka kwa watu wa Manase, Efuraimu na kutoka pande zingine zote za Israeli, inchi ya Yuda yote na ya Benjamina, na vilevile kutoka kwa wenyeji wa Yerusalema.


Tena wakati wa utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia, Bisilamu, Mitiredati, Tabeli na warafiki zao, wakamwandikia barua mufalme Artasasta. Barua hiyo iliandikwa katika herufi za Kiaramea na kutafsiriwa.


Viongozi wa Wayuda waliendelea vizuri sana na kazi ya ujenzi wa hekalu, wakitiwa moyo na nabii Hagai na Zakaria mwana wa Ido. Wakamaliza ujenzi wa hekalu kama walivyoamriwa na Mungu wa Israeli, na kama walivyoagizwa na mufalme Kiro, mufalme Dario na mufalme Artasasta, wa Persia.


Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza Sheria ya Yawe, kuitii na kuwafundisha watu wa Israeli masharti na maagizo zake.


Mimi Artasasta, mufalme wa wafalme, ninatuma barua hii kwa Ezra, kuhani na mutu mwenye ujuzi katika Sheria ya Mungu wa mbinguni.


mwana wa Salumu mwana wa Zadoki mwana wa Ahitubu


Mimi mufalme Artasasta, ninatoa amri kwa walinzi wa hazina wote katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kwamba kitu chochote Ezra atakachohitaji, kuhani na mwandishi wa Sheria ya Mungu wa mbinguni, mutamupa, tena bila kusita,


Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Mesulamu mwana wa Zadoki mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya Mungu,


Katika mwezi wa Nisani, kwa mwaka wa makumi mbili wa utawala wa mufalme Artasasta, wakati divai ilipokuwa mbele yake, nilitwaa divai na kumupatia mufalme. Mpaka sasa nilikuwa sijapata kuwa na huzuni mbele yake.


Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ