Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kila siku, tena bila kukosa, mutawapa makuhani wa Yerusalema kila kitu watakachohitaji; ikuwe ni ngombe dume, wana-ngombe, kondoo dume au wana-kondoo wa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Mungu wa mbinguni, au ngano, chumvi, divai au mafuta.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 6:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wengine walichaguliwa kusimamia vifaa vya hekalu, na vyombo vyote vitakatifu, na unga safi, divai, mafuta ya mizeituni, ubani na marasi.


Haya yote yatatendeka kusudi waweze kumutolea Mungu wa mbinguni sadaka zinazomupendeza na waombee maisha yangu mimi mufalme na watoto wangu.


Zaidi ya hayo, ninatoa amri kwamba ninyi mutawasaidia katika kazi hiyo. Mali zao zote walizotumia zitalipwa bila kuchelewa kutoka katika hazina ya mufalme inayotokana na kodi kutoka katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Musa akamwambia Haruni: Twaa mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, nyama wote wasikuwe na kilema. Kisha uwatoe sadaka mbele ya Yawe.


“Kwa maana kila mutu atatiwa chumvi kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ