Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 6:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, watu wa Israeli, makuhani, Walawi na watu wengine waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho wakaizindua nyumba ya Mungu kwa shangwe kubwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 6:16
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mufalme Solomono na Waisraeli wote waliokuwa pamoja naye walimutolea Yawe sadaka.


Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika pamoja kwa shangwe kwa kubeba Sanduku la Agano la Yawe mpaka Yerusalema. Wakalisindikiza kwa mulio wa baragumu, ngunga, matoazi, na sauti kubwa za vinanda na vinubi.


Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


watu waliamua kwa shauri moja kuendelesha sherehe kwa muda wa siku saba zaidi. Basi wakaendelea kusherehekea kwa furaha kubwa kwa muda wa siku saba zaidi.


Kukakuwa furaha kubwa sana Yerusalema, maana tangu wakati wa mufalme Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli jambo kama hilo lilikuwa halijatokea Yerusalema.


Naye Solomono akamutolea ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja makumi mbili. Hivi ndivyo Solomono na watu wote walivyozinduwa nyumba ya Mungu.


Kisha waadui za watu wa Yuda na Benjamina waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka katika uhamisho wanalijenga upya hekalu la Yawe, Mungu wa Israeli,


Kwa muda wa siku saba watu walisherehekea kwa furaha sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa sababu Yawe aliwajalia furaha na kumupa mufalme wa Asuria moyo wa upendo kwao, akawasaidia katika kazi za ujenzi wa nyumba ya Mungu, wa Israeli.


Kisha wakati wa kuzindua ukuta wa Yerusalema Walawi wakatafutwa kila pahali walipokaa kwa kuja Yerusalema kusherehekea kwa furaha pamoja na shukrani na nyimbo, wakitumia matoazi, vinubi na zeze.


Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.


Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Wimbo wa Safari za kidini. Wa Daudi. Nilifurahi waliponiambia: “Twende kwenye nyumba ya Yawe.”


Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?


Siku moja, katika nyakati za mvua kubwa, kukakuwa sikukuu ya Kukumbuka Muzinduo wa hekalu katika Yerusalema.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ