Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mungu aliyeuchagua Yerusalema kuwa pahali pake pa kuabudiwa amwangushe mufalme au taifa lolote litakalopinga amri hii au kutaka kuiharibu nyumba hii ya Mungu inayokuwa katika Yerusalema. Ni mimi Dario niliyetoa amri hii na inapaswa kushikwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 6:12
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alimwambia: “Nimesikiliza wakati uliponiomba na kunisihi. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umenijengea kusudi watu waabudu jina langu hapa milele. Nitaichunga na kuipenda wakati wote.


kwa maana nimetakasa nyumba hii kusudi watu waliabudu jina langu hapa milele. Nitailinda na kuipenda siku zote.


Basi, Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi, na wakubwa wenzao, wakafanya bidii kwa kutimiza maagizo ya mufalme.


Viongozi wa Wayuda waliendelea vizuri sana na kazi ya ujenzi wa hekalu, wakitiwa moyo na nabii Hagai na Zakaria mwana wa Ido. Wakamaliza ujenzi wa hekalu kama walivyoamriwa na Mungu wa Israeli, na kama walivyoagizwa na mufalme Kiro, mufalme Dario na mufalme Artasasta, wa Persia.


Utatwaa feza na zahabu ambayo mimi na washauri wangu tumemutolea kwa utashi wetu Mungu wa Israeli ambaye hekalu lake liko katika muji Yerusalema.


Feza hiyo utaitumia kwa uangalifu sana kwa kununua ngombe dume, kondoo dume, wana-kondoo na sadaka ya unga na divai, na kuvitoa kwenye mazabahu katika nyumba ya Mungu wenu inayokuwa Yerusalema.


Mutu yeyote ambaye hatatii Sheria ya Mungu wako na ya mufalme, ahukumiwe mara moja: kufa, kuhamishwa, kunyanganywa mali yake au kufungwa.


Kwa amri ya mufalme, wajumbe waliopanda juu ya farasi wa kifalme wenye nguvu wanaokimbia mbio, wakaondoka mbio. Tangazo hili vilevile lilitolewa katika muji mukubwa Susani.


Ndani ya vinywa vyao hamuna ukweli wowote; mioyo yao imejaa maangamizi, koo zao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu.


Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamizwa; mataifa hayo yatateketezwa kabisa.


Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.


Naye akauliza: “Wewe ni nani, Bwana?” Na Bwana akajibu: “Mimi ni Yesu unayemutesa.


basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.


Lakini mutakwenda pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, atachagua katika makabila yote kwa kuweka jina lake na makao yake hapo. Huko ndiko mutakakokwenda.


Mutatoa sadaka ya Pasaka kutoka mifugo yenu ya kondoo au ngombe kwa heshima ya Yawe pahali ambapo Yawe atachagua kwa ajili ya jina lake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ