Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 5:8
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake.


Walimutumia mufalme barua iliyoandikwa hivi: Kwa mufalme Dario, tunakutakia amani.


Tuliwauliza viongozi hao watuambie ni nani aliyewapa amri ya kuijenga upya nyumba hii mpaka kuimaliza.


Haya yote yatatendeka kusudi waweze kumutolea Mungu wa mbinguni sadaka zinazomupendeza na waombee maisha yangu mimi mufalme na watoto wangu.


Kuta zake zitajengwa kwa mustari mumoja wa miti juu ya kila mistari tatu ya mawe makubwa. Mali itakayotumiwa kwa kazi ile itatoka katika hazina ya mufalme.


Kila kitu Mungu wa mbinguni alichoagiza kwa ajili ya nyumba yake, kinapaswa kutimizwa kikamilifu, kusudi asipate kukasirikia ufalme wangu au wana wangu.


Na katika miji mingine, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango na wazao wa watumishi wa Solomono, walikaa katika maeneo yao wenyewe, katika miji yao.


Wale waliokuwa katika uhamisho kule Babeli, walirudi Yerusalema na katika inchi ya Yuda, kila mumoja akarudi katika muji wake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babeli tangu mufalme Nebukadneza alipowahamishia kule wakiwa watumwa.


Mufalme Ahasuero alipotawala ufalme wake ulikuwa na majimbo mia moja makumi mbili na saba, toka Uhindi mpaka Etiopia.


Basi, akapeleka barua kwa kila jimbo kwa luga na maandiko yanayoeleweka katika jimbo: kwamba kila mwanaume akuwe bwana wa nyumba yake, na kuitangaza habari hii kwa luga yake.


Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi; ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.


Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.


Halafu mufalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na luga zote katika dunia: Ninawatakia amani kwa wingi.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Hata waadui zetu wenyewe wanajua wazi, mulinzi wao hana nguvu kama mulinzi wetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ