Kisha mufalme akatuma jibu hili: Kwa mutawala Rehumu, kwa Simusayi, karani wa jimbo, pamoja na wenzenu wote wanaoishi Samaria na pahali pengine katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.
Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.
Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni: Danieli, mutumishi wa Mungu Mwenye Uzima, Mungu wako unayemutumikia siku zote ameweza kukuokoa na simba hawa?