Mara tu waliposomewa barua hii kutoka kwa Artasasta, Rehumu, karani Simusayi na wenzao wakaharakisha kwenda Yerusalema na kuwalazimisha kwa nguvu Wayuda waache kuujenga muji.
Hii barua inatoka kwa mutawala Rehumu na kwa Simusayi, karani wa jimbo pamoja na wenzetu, na waamuzi, wakubwa wote ambao pale mbele walitoka Ereki, Babeli, Susani, Dini, Afarsati, Terpeli, Deha na Elamu,
Kisha Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wenzao, wakakwenda Yerusalema na kuuliza: “Nani aliyewaamuru kuijenga nyumba hii mpaka kuimaliza?”
Halafu Dario akatuma ujumbe huu: Kwa Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wakubwa wenzako katika jimbo. Musiende kule kwenye hekalu,
Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.