Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 5:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Vilevile akavirudisha vyombo vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevipeleka kutoka katika hekalu kule Yerusalema na kuviweka katika hekalu la Babeli. Vyombo hivyo Kiro akaviondoa toka hekalu la Babeli na kuvipatia Sesebasari ambaye alikuwa amemuchagua akuwe mutawala wa Yuda; akamwamuru akisema:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 5:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Nebukadneza akatwaa vilevile vyombo vimoja vya nyumba ya Yawe akavipeleka Babeli na kuviweka katika nyumba ya kifalme kule Babeli.


“Utwae vyombo hivyo na kuvirudisha katika hekalu la Yerusalema, na kuijenga upya nyumba ya Mungu pahali pake.”


Kisha Sesebasari akakuja na kuweka musingi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema, na tangu wakati huo ujenzi umekuwa ukiendelea mpaka sasa, lakini bado haujamalizika.


Vilevile, vyombo vyote vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alivileta Babeli kutoka katika hekalu la Yerusalema, vitarudishwa na kuwekwa kila kimoja pahali pake katika nyumba ya Mungu.”


Ezra akasema: “Asifiwe Yawe, Mungu wa babu zetu, ambaye amemupatia mufalme moyo wa kupamba nyumba ya Yawe inayokuwa Yerusalema.


Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.


Yule mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme alipeleka vibakuli, vyetezo, mabeseni, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya zahabu au vya feza.


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Basi, Yawe akamutia moyo mutawala Zerubabeli wa Yuda pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho. Wakaanza kazi hiyo ya kuijenga upya nyumba ya Yawe wa majeshi, Mungu wao,


Sema na mutawala wa Yuda, Zerubabeli mwana wa Saltieli, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki na watu waliorudi kutoka katika uhamisho uwaambie hivi:


Sema na Zerubabeli mutawala wa Yuda umwambie hivi: Nitazitikisa mbingu na dunia


Yule liwali alipoona mambo yale yaliyotokea, akashangaa na mafundisho ya Bwana hata akapata kumwamini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ