Ezra 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Wakati ule, manabii wawili, Hagai na Zakaria mwana wa Ido, wakawatolea unabii Wayuda waliokuwa wanakaa Yuda na Yerusalema, katika jina la Mungu wa Israeli.
Viongozi wa Wayuda waliendelea vizuri sana na kazi ya ujenzi wa hekalu, wakitiwa moyo na nabii Hagai na Zakaria mwana wa Ido. Wakamaliza ujenzi wa hekalu kama walivyoamriwa na Mungu wa Israeli, na kama walivyoagizwa na mufalme Kiro, mufalme Dario na mufalme Artasasta, wa Persia.
Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.
Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:
Sasa, mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Leo ni siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, siku ambayo musingi wa hekalu umekamilika. Basi mufikiri vizuri:
Yawe wa majeshi anasema hivi: Mujipe moyo! Sasa munayasikia maneno ambayo mulitangaziwa na manabii wakati musingi wa hekalu langu ulipowekwa kulijenga upya.