Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 4:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Wafalme wenye nguvu wamepata kuutawala muji ule pamoja na jimbo la upande wa magaribi wa Furati wakilipisha kodi, malipo ya kuvuka mipaka na mengine.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 4:20
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Solomono alitawala falme zote kuanzia kwa muto Furati mpaka katika inchi ya Wafilistini, na kuendelea hata kwa mupaka na Misri. Mataifa yote yalimutumikia na kulipa kodi kwake wakati wote wa maisha yake.


Inchi yote upande wa magaribi wa muto Furati, kutokea Tifusa mpaka muji wa Gaza, ilikuwa chini ya utawala wake. Wafalme wote upande wa magaribi wa muto Furati walikuwa chini yake, na alikuwa na amani na inchi zote jirani.


Basi akaweka kambi za waaskari kule Edomu. Nao Waedomu wote wakakuwa watumishi wa Daudi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Daudi akamushinda vilevile Hadadezeri mufalme wa Zoba, inchi iliyokuwa karibu na Hamati, alifanya hivyo wakati alipokuwa akienda kujisimamishia nguzo ya ukumbusho kwenye sehemu za muto Furati.


Halafu Daudi akaweka kambi za waaskari katika muji wa Damasiki wa Aramu. Basi Waaramu wakakuwa watumishi wake, na wakakuwa wanalipa kodi. Yawe akamupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Kisha watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi nao wakakuwa watumishi wa Daudi. Halafu Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.


Vilevile Wafilistini wamoja wakamuletea Yosafati zawadi pamoja na feza nyingi na Waarabu wengine nao wakamuletea kondoo dume elfu saba na mia saba, na mbuzi dume elfu saba na mia saba.


zaidi ya zahabu aliyopokea kutoka kwa wafanya biashara na wachuuzi, tena kutoka kwa wafalme wote wa Arabia na watawala wa inchi ya Israeli.


Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba muji huu ukijengwa upya na kuta zake zikimalizika, watu hawatalipa kodi, malipo ya kuvuka mipaka, na mengine mbalimbali na hazina yako itapunguka.


Kwa hiyo tunakujulisha kwamba ikiwa muji huu utajengwa upya na kuta zake zikimalizika, hautaweza kutawala jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Nimetoa amri uchunguzi ufanyike na imegunduliwa kuwa ni kweli kwamba tangu zamani muji huu wa Yerusalema umekuwa ukiwapinga wafalme na kwamba watu wake wamekuwa waasi na wachochezi wakubwa.


Kwa hiyo, mutoe amri watu hao waache kuujenga upya muji ule mpaka pale nitakapotoa maagizo mengine.


Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.


Atawale kutoka bahari hata bahari, kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.


Namna gani muji uliokuwa umejaa watu, sasa unakaa peke yake! Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa, sasa umekuwa kama mama mujane. Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji, sasa umekuwa mutumwa.


Ulikuwa na matawi yenye nguvu, ambayo yalikuwa fimbo za kifalme. Muzabibu huo ulikomaa kupita miti mingine, watu walisifu ukubwa wa shina lake na wingi wa matawi yake.


Yesu alipokuwa akipita, akamwona mutu anayeitwa Matayo, akiikaa katika nyumba ya kulipishia kodi. Yesu akamwambia: “Unifuate!” Naye akasimama na kumufuata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ