Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 3:7
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.


Solomono alikuwa na vibanda elfu makumi ine kwa ajili ya farasi wa magari yake ya kukokotwa, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili.


Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.


kwa wajengaji na wenye kuchonga mawe, na zikatumiwa kwa kununua mbao na mawe yaliyochongwa kwa kutengeneza nyumba ya Yawe na kutimiza mahitaji mengine yote ya kazi ya kutengeneza nyumba.


Zikawekwa katika mikono ya wale wafundi waliosimamia kazi ya kutengeneza nyumba ya Yawe; na wafundi waliofanya kazi katika nyumba ya Yawe wakazitoa kwa kutengeneza na kufanya upya nyumba.


Ingawa musingi wa hekalu la Yawe ulikuwa bado kuwekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


Hata watu wa inchi ya Yuda na ya Israeli walifanya biashara nawe; walikupa ngano, mizeituni, tini za kwanzakwanza, asali, mafuta na marasi kwa kununua vitu kwako.


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Herode alikuwa amechunga hasira sana juu ya watu wa muji Tiro na wa Sidona. Lakini wakapatana kwa nia moja kwa kumwendea. Kwanza wakasikilizana na Balasto, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya mufalme. Kisha wakaomba mapatano ya amani kwa mufalme Herode, kwa sababu inchi yao ilitegemea inchi ya mufalme huyo kwa kupata chakula.


Katika muji wa Yopa kulikuwa mwanafunzi mumoja mwanamuke aliyeitwa Tabita. (Katika kigriki ni “Dorika,” maana yake “Pongo”.) Mwanamuke huyu alikuwa akifanya matendo mengi mema na kuwasaidia wamasikini.


Na kwa kuwa muji Luda ulikuwa karibu na muji Yopa, wanafunzi walikuwa wamesikia kwamba Petro yuko kule. Kwa hiyo wakatuma kwake wajumbe wawili kwa kumwambia: “Tunakusihi, ufike huku kwetu bila kukawia.”


Petro akakaa siku nyingi huko Yopa kwa fundi mumoja wa kutengeneza vitu vya ngozi, aliyeitwa Simoni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ