Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Walitoa vilevile sadaka za kawaida ambazo ziliteketezwa nzima, sadaka zilizotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi na katika sikukuu nyingine zote alizoagiza Yawe. Vilevile walitoa sadaka zote za mapenzi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 3:5
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kore mwana wa Imuna, Mulawi, aliyekuwa mulinzi wa Mulango wa Mashariki wa hekalu, akasimamia matoleo yote ya mapenzi kwa Mungu; na kugawanya matoleo kwa ajili ya Yawe na sadaka zinazokuwa takatifu kabisa.


Ingawa musingi wa hekalu la Yawe ulikuwa bado kuwekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


kwa ajili ya mikate mitakatifu, sadaka za unga za kawaida, sadaka za kuteketezwa kwa moto za kawaida, sadaka za siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, sikukuu nyingine zilizowekwa, vitu vingine vitakatifu, sadaka za kusamehewa zambi, kwa kuwafanyia upatanisho watu wa Israeli na kazi nyingine zozote za nyumba ya Mungu wetu.


Vilevile nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwa pale siku zote kwa kunitumikia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga na kunitolea sadaka milele.


Uwaambie Waisraeli kwamba kama mutu anapenda kumutolea Yawe sadaka ya nyama, nyama huyo atamuchagua kutoka kundi lake la ngombe, kondoo au mbuzi.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Uwaambie Waisraeli hivi: Katika sikukuu zangu mimi Yawe ambazo zimepangwa mutakuwa na mukutano mutakatifu. Sikukuu ambazo nimepanga ni hizi:


Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni litre mbili za divai kwa kila ngombe dume; litre moja na nusu kwa kila kondoo dume, na litre moja kwa kila mwana-kondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka muzima.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kama vile sadaka ya ngano kwa Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe bila kilema.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote hao wakuwe bila kilema.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: wana-ngombe dume kumi na watatu, kondoo dume wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.


Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe wasiokuwa na kilema chochote.


Haya ndiyo maagizo juu ya sadaka mutakazomutolea Yawe wakati wa sikukuu zenu zilizopangwa. Zaidi ya hizi zote, kuna vilevile sadaka za kuteketezwa, za vyakula na za kinywaji, za kutimiza kiapo na za mapenzi, na za amani.


Mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu ya kumupendeza Yawe: mwana-ngombe mumoja, kondoo dume mumoja, wana-kondoo saba wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.


Musikule vitu hivi pahali munapoishi: sehemu ya kumi za ngano zenu, divai zenu au mafuta yenu, wazaliwa wa kwanza wa ngombe wenu au kondoo wenu, au sadaka zenu za kutimiza kiapo au za mapenzi, au matoleo mengine.


Vilevile huko mutapeleka sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, matoleo yenu ya mapenzi na ya kutimiza kiapo, na wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ