Ezra 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Wakafanya sikukuu ya vibanda kama ilivyoandikwa katika Sheria; kila siku walitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizohitajika kwa ajili ya siku hiyo.
Halafu, mufalme Daudi akawaacha Asafu na wandugu zake Walawi pahali walipoliweka Sanduku la Agano la Yawe, kwa ajili ya kazi zinazotakiwa mbele ya sanduku kila siku.
Tena, bila kujali ukoo walimoandikishwa, waliwapa sehemu wale watoto wa kiume waliokuwa wametimiza umri wa miaka mitatu na zaidi, na ambao waliingia katika nyumba ya Yawe kila siku kwa kutimiza kazi zao. Kila mumoja wao alipata sehemu yake kulingana na kazi aliyofanya kwa zamu yake.
Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.
Haya ndiyo maagizo juu ya sadaka mutakazomutolea Yawe wakati wa sikukuu zenu zilizopangwa. Zaidi ya hizi zote, kuna vilevile sadaka za kuteketezwa, za vyakula na za kinywaji, za kutimiza kiapo na za mapenzi, na za amani.