Ezra 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20022 Yesua mwana wa Yosadaki, pamoja na makuhani wenzake, na Zerubabeli, mwana wa Sealtieli, pamoja na wandugu zake, wakaijenga upya mazabahu ya Mungu wa Israeli, kusudi waweze kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutu wa Mungu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Basi, watu wakaanza kazi katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili nyuma ya kufikia kwenye nyumba ya Mungu katika Yerusalema. Zerubabeli, mwana wa Saltieli, Yesua mwana wa Yosadaki, wandugu zao wengine, makuhani, Walawi na watu wengine wote waliorudi Yerusalema kutoka katika uhamisho, wakajiunga nao katika kazi hiyo. Walawi wote waliokuwa na umri wa miaka makumi mbili au zaidi, walichaguliwa kwa kusimamia kazi ya kuijenga upya nyumba ya Yawe.
Haya ndiyo majina ya makuhani na Walawi waliorudi toka katika uhamisho pamoja na Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Kuhani Mukubwa Yesua. Makuhani walikuwa: Seraya, Yeremia, Ezra, Amaria, Maluku, Hatusi, Sekania, Rehumu, Meremoti, Ido, Ginetoni, Abiya, Miyamini, Madia, Bilga, Semaya, Yoyaribu, Yedaya, Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hao walikuwa ni wakubwa wa makuhani na wandugu zao wakati wa Yesua.