Kisha kuhani Zadoki na nabii Natani wakamupakaa mafuta akuwe mufalme kule Gihoni. Halafu wametoka hapo wakifurahi, ndiyo sababu ya makelele hayo unayosikia.
Wengi kati ya makuhani, Walawi, na viongozi wa ukoo waliokuwa wazee na ambao walikuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakalia kwa sauti kubwa walipouona musingi wa nyumba hii mupya unawekwa, ingawa watu wengine wengi walipaza sauti kwa furaha.
Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.
sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.
Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!