Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Watu hawakuweza kutofautisha kati ya sauti za furaha na za kilio kwa sababu zilikuwa nyingi na zilisikilika mbali sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 3:13
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu watu wote walimufuata, wakipiga mazomari, wakafurahi kwa shangwe kubwa, hata inchi ikatikisika kwa sauti zao.


Kisha kuhani Zadoki na nabii Natani wakamupakaa mafuta akuwe mufalme kule Gihoni. Halafu wametoka hapo wakifurahi, ndiyo sababu ya makelele hayo unayosikia.


Wengi kati ya makuhani, Walawi, na viongozi wa ukoo waliokuwa wazee na ambao walikuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakalia kwa sauti kubwa walipouona musingi wa nyumba hii mupya unawekwa, ingawa watu wengine wengi walipaza sauti kwa furaha.


Kisha waadui za watu wa Yuda na Benjamina waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka katika uhamisho wanalijenga upya hekalu la Yawe, Mungu wa Israeli,


Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.


Ee Mungu, uwaazibu kwa makosa yao, waanguke katika mipango yao wenyewe; uwafukuze inje kwa sababu ya zambi zao nyingi, kwa sababu wamekuasi wewe.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Siku hizo na wakati huo, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kuja wakilia na kutafuta Yawe, Mungu wao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


Wakapaita pahali pale Bokimu, ni kusema “Wanaolia”. Pale wakamutolea Yawe sadaka.


Sanduku la Agano la Yawe lilipofika katika kambi Waisraeli wote walishangilia kwa furaha, hata inchi yote ikatikisika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ