Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wajengaji walipoanza kuweka musingi wa hekalu la Yawe, makuhani wakiwa wamevaa nguo zao, walisimama pahali pao na baragumu katika mikono, nao Walawi wa ukoo wa Asafu wakisimama na matoazi yao, basi, wakamutukuza Yawe kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi wa Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 3:10
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sebania, Yosafati, Netaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, waliokuwa makuhani, waliwekwa kwa kupiga baragumu mbele ya Sanduku la Agano. Obedi-Edomu na Yehiya waliwekwa vilevile kuwa walinzi wa sanduku.


Daudi alikuwa akivaa kanzu ya kitani safi, hata vilevile na Walawi wote waliobeba sanduku, waimbaji na Kenania kiongozi wa waimbaji. Zaidi ya kanzu ile, Daudi alikuwa akivaa kizibao cha kitani.


Halafu, mufalme Daudi akawaacha Asafu na wandugu zake Walawi pahali walipoliweka Sanduku la Agano la Yawe, kwa ajili ya kazi zinazotakiwa mbele ya sanduku kila siku.


Hemani na Yedutuni walikuwa na baragumu na matoazi kwa ajili ya muziki na ala za muziki kwa ajili ya nyimbo takatifu. Wana wa Yedutuni walichaguliwa kwa kulinda milango.


elfu ine wakuwe walinzi wa milango, na elfu ine wakuwe waimbaji, wakimusifu Yawe kwa ala za muziki mufalme alizotengeneza mwenyewe kwa ajili ya kazi hiyo.


Kisha, Walawi wakafanya matayarisho kwa ajili yao wenyewe na kwa makuhani kwa maana makuhani wa uzao wa Haruni walikuwa wanashugulika na kutoa sadaka za kuteketeza kwa moto, na vipande vya mafuta, mpaka usiku; kwa hiyo Walawi walitayarisha kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Haruni.


Nao waimbaji wa uzao wa Asafu wakashika nafasi zao, kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi, Asafu, Hemani na Yedutuni, nabii wa mufalme. Nao walinzi wa mulango walikuwa kwenye milango; hawakuhitajika kuacha nafasi zao za kazi kwa sababu wandugu zao Walawi waliwatayarishia Pasaka.


Walawi wote waimbaji, pamoja na Asafu, Hemani, na Yedutuni, pamoja na Walawi wengine wa ukoo zao, wakiwa wamevaa nguo zao za kitani safi nao wakabeba matoazi, vinanda na vinubi, walisimama upande wa mashariki wa mazabahu. Makuhani mia moja na makumi mbili wapiga baragumu walikuwa pamoja nao.


Waimbaji (wazao wa Asafu), walikuwa mia moja makumi mbili na wanane.


Kisha Sesebasari akakuja na kuweka musingi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema, na tangu wakati huo ujenzi umekuwa ukiendelea mpaka sasa, lakini bado haujamalizika.


Mumusifu kwa matoazi ya sauti kubwa, mumusifu kwa matoazi yenye kuvuma sana!


Lakini sasa mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Mbele ya kuanza kujenga upya nyumba yangu,


Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?


Kwa hiyo, mufalme Saulo akamwambia Doegi: “Wewe geuka uwaue makuhani.” Doegi Mwedomu akaenda na kuwaua makuhani wote. Siku hiyo, Doegi aliua makuhani makumi nane na watano ambao wanavaa vizibao vya kikuhani vya kitani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ