Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 2:68 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

68 Watu hao waliotoka katika uhamisho, walipofika kwenye nyumba ya Yawe katika Yerusalema, viongozi wamoja wa ukoo hizo walitoa matoleo ya mapenzi kwa kusaidia ujenzi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 2:68
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu malaika wa Yawe akamwamuru Gadi amwambie Daudi aende kumujengea Yawe mazabahu, katika kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani wa kabila ya Yebusi.


Basi Daudi akasema: “Hapa ndipo pahali ambapo nyumba ya Yawe itakuwa, na hii ndiyo mazabahu ambapo watu wa Israeli watatolea sadaka ya kuteketezwa kwa moto.”


Kisha Solomono akaanza kujenga nyumba ya Yawe katika Yerusalema juu ya mulima Moria ambapo Yawe alimutokea Daudi baba yake, pahali ambapo Daudi alikuwa amepachagua, kwenye kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani Muyebusi.


Walitoa kila mutu kadiri ya uwezo wake kwa ajili ya kazi hii. Jumla ya matoleo hayo ilikuwa kilo mia tano za zahabu, kilo elfu mbili na mia nane za feza na nguo mia moja kwa ajili ya makuhani.


Wakaijenga mazabahu hiyo pahali palepale ilipokuwa hapo zamani, kwa kuwa waliwaogopa watu waliokuwa wanaishi katika inchi hiyo. Kisha wakakuwa wanamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake kila siku asubui na magaribi.


Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


Uwaambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo. Utapokea matoleo kutoka kwa mutu yeyote atakayetoa kwa moyo safi.


Kila mutu aliyevutwa na kusukumwa ndani ya moyo wake alimutolea Mungu muchango wake kwa ajili ya hema la mukutano, kazi zake zote na nguo yake takatifu.


Waisraeli wote, wanaume na wanawake, ambao walivutwa ndani ya moyo wao kuleta kitu chochote kwa ajili ya kazi ambayo Yawe alikuwa amemwagiza Musa ifanyike, walileta vitu hivyo kwa mapenzi yao, kama vile muchango wa kumupa Yawe.


Hao wakapokea kutoka kwa Musa vitu vyote vilivyotolewa na Waisraeli kwa mapenzi yao kwa ajili ya kazi ya hema takatifu. Watu waliendelea kumuletea michango yao kufuatana na mapenzi yao kila asubui.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Ninayashuhudia kwamba kwa mapenzi yao yalitoa kwa kadiri yalivyoweza na hata zaidi kupita uwezo wao.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ