Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 2:1
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nebuzaradani, mukubwa wa waaskari wa mufalme, akawapeleka katika uhamisho watu waliokuwa wamebakia katika muji na wale wote waliokuwa wamejitoa wenyewe kwa mufalme wa Babeli pamoja na watu wengine wote.


Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu.


Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu.


Vyombo vyote vya zahabu na feza, pamoja na vitu vingine vilikuwa jumla yake elfu tano mia ine. Vyote hivi, Sesebasari alivibeba mpaka Yerusalema wakati yeye pamoja na watu wengine walipotolewa toka katika uhamisho kule Babeli kwenda Yerusalema.


Viongozi wao walikuwa Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Seraya, Relaya, Mordekayi, Bilsani, Misipari, Bigwayi, Rehumu na Bana. Hii ndiyo hesabu ya watu wote wa ukoo za Waisraeli waliorudi kutoka katika uhamisho:


Basi, makuhani, Walawi na watu wengine wamoja wakaanza kuishi katika Yerusalema na katika vijiji vyake. Nao waimbaji, walinzi wa hekalu na watumishi wa hekalu wakaanza kuishi katika miji yao; Waisraeli wote wakaishi katika miji yao.


Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.


Lakini kitabu kikapatikana katika muji wa Akimeta katika jimbo la Media, nacho kilikuwa na maagizo haya:


Kisha, watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakamutolea Mungu wa Israeli sadaka zao za kuteketezwa kwa moto. Wakatoa ngombe dume kumi na wawili kwa ajili ya Israeli yote, kondoo dume makumi kenda na sita na wana-kondoo makumi saba na saba; vilevile walitoa mbuzi kumi na wawili kama sadaka ya kusamehewa zambi. Nyama wote hawa walitolewa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.


Haya ndiyo majina ya makuhani na Walawi waliorudi toka katika uhamisho pamoja na Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Kuhani Mukubwa Yesua. Makuhani walikuwa: Seraya, Yeremia, Ezra, Amaria, Maluku, Hatusi, Sekania, Rehumu, Meremoti, Ido, Ginetoni, Abiya, Miyamini, Madia, Bilga, Semaya, Yoyaribu, Yedaya, Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hao walikuwa ni wakubwa wa makuhani na wandugu zao wakati wa Yesua.


Mufalme Ahasuero alipotawala ufalme wake ulikuwa na majimbo mia moja makumi mbili na saba, toka Uhindi mpaka Etiopia.


Akawaamuru hao wamuletee malkia Vashiti, akiwa amevaa taji yake ya kimalkia. Malkia yule alikuwa na sura nzuri sana, hivyo mufalme alitaka kuwaonyesha wageni wake na viongozi uzuri wake.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.


Kila mutu alikunywa sawa vile alivyotaka; mufalme alikuwa ametoa maagizo kwa watumishi wa nyumba ya kifalme wamutendee kila mutu kadiri ya mahitaji yake.


Basi, katika siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa tatu inayoitwa Siwani, Mordekayi akawaita waandishi wote wa mufalme, akawaagiza waandike barua kwa Wayuda na wakubwa, watawala na wakubwa wa majimbo yote mia moja makumi mbili na saba, kuanzia Uhindi mpaka Etiopia. Barua hizo zikaandikwa kwa kila jimbo katika luga yake na sawasawa na maandiko yake, vilevile na kwa Wayuda kwa maandiko yao na luga yao.


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Nitawarudisha Waisraeli katika inchi yao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mulima Karmeli na Basani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efuraimu na Gileadi.


Watu wa Yuda wamekwenda katika uhamisho, wakijaa mateso na kuwa katika utumwa mukali. Wanakaa kati ya watu wa mataifa, wala hawapati nafasi ya kupumzikia. Waliowafuatilia wamewakamata wakiwa katika taabu.


Waadui zake ndio wanaoutawala na wanafanikiwa, maana Yawe ameutesa kwa sababu ya makosa yake mengi. Watoto wake wanapelekwa katika uhamisho.


Azabu ya uovu wako, ewe Sayuni imekamilika; Yawe hatawaacha zaidi katika uhamisho. Lakini ninyi Waedomu atawaazibu kwa uovu wenu, atazifichua zambi zenu.


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Liwali akasoma barua ile na kumwuliza Paulo: “Wewe ni mutu wa jimbo gani?” Aliposikia kwamba yeye ni mutu wa jimbo la Kilikia,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ