Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 10:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 10:8
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tangazo likatolewa kila pahali katika inchi ya Yuda na Yerusalema kwa wote waliotoka katika uhamisho kwamba wakusanyike Yerusalema.


Katika siku hizo tatu, kwa siku ya makumi mbili ya mwezi wa tisa, watu wote walioishi katika majimbo ya Yuda na Benjamina wakafika Yerusalema na kukusanyika katika kiwanja cha nyumba ya Mungu. Watu wote walikuwa wakitetemeka kwa sababu ya shauri waliloitiwa na kwa ajili ya mvua nyingi iliyokuwa ikinyesha.


Mutu yeyote ambaye hatatii Sheria ya Mungu wako na ya mufalme, ahukumiwe mara moja: kufa, kuhamishwa, kunyanganywa mali yake au kufungwa.


Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.


Watu wa Israeli waliposikia Sheria hiyo wakawatenga watu wa mataifa mengine.


Lakini kitu chochote kilichotakaswa kwa Yawe, kama ni mutu au nyama au kitu kilichopatikana kwa urizi, hakitauzishwa wala kukombolewa. Chochote kilichotakaswa kwa Yawe ni kitakatifu kabisa.


Na kama akikataa kuwasikia watu wale, upeleke habari kwa kanisa. Naye akikataa kusikia kanisa vilevile, umuhesabu kama mupagani na mutenda maovu sawa walipishaji wa kodi.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Lakini feza yote, zahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Yawe; hivyo vitawekwa katika hazina ya Yawe.”


Kisha wakaulizana: “Kati ya makabila yote ya Israeli kuna kikundi chochote ambacho hakikuhuzuria mukutano uliofanyika mbele ya Yawe?” Walikuwa wamefanya kiapo kwamba mutu yeyote ambaye hatahuzuria mbele ya Yawe kule Misipa anapaswa kuuawa.


Akatwaa ngombe dume wawili, akawakatakata vipande, akatuma wajumbe wapitishe vipande hivyo katika mipaka yote ya Waisraeli wakisema: “Mutu yeyote ambaye hatamufuata Saulo na Samweli katika vita, ngombe dume wake watafanyiwa hivyo.” Waisraeli waliingiwa na hofu juu ya kile ambacho Yawe angeweza kufanya. Kwa hiyo, wote walitoka pamoja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ