Sasa, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa nia na moyo wote. Basi mujitayarishe kumujengea Yawe pahali patakatifu kusudi Sanduku la Agano la Yawe pamoja na vyombo vyote vitakatifu vinavyotumiwa katika ibada, viwekwe ndani ya nyumba iliyojengwa kwa ajili ya Yawe.”
Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.
Makuhani na Walawi wamekwisha kupangiwa kazi watakazofanya katika nyumba ya Mungu. Watumishi wenye ujuzi wa kila aina watakuwa tayari kabisa kukusaidia, na watu wote pamoja na viongozi wao watakuwa chini ya mamlaka yako.”
Ezra akasimama na kuanza kuwaapiza makuhani, viongozi, Walawi na Waisraeli wengine wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa, nao wakakubali kufanya kiapo.
Itakuwa kama vile mutu anayefunga safari. Alipotoka kwake akawaachia watumishi madaraka yake, akimupa kila mutu kazi yake. Vilevile akamwagiza mulinzi wa mulango akeshe.