Sasa, mutubu zambi zenu mbele ya Yawe, Mungu wa babu zenu, na kufanya yale yanayomupendeza. Mujitenge na wakaaji wa inchi hii na kuwaacha wake zenu wa kigeni.”
Lakini wakaongeza kusema: “Watu ni wengi na mvua inanyesha sana. Hatuwezi kuendelea kusimama hapa katika kiwanja, na hili si jambo ambalo litamalizika kwa siku moja au mbili! Tumefanya kosa kubwa sana juu ya shauri hili.