Ezra 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Sasa, mutubu zambi zenu mbele ya Yawe, Mungu wa babu zenu, na kufanya yale yanayomupendeza. Mujitenge na wakaaji wa inchi hii na kuwaacha wake zenu wa kigeni.”
Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,
Kwa hiyo, tufanye agano na Mungu wetu, tuachane na wanawake hawa pamoja na watoto wao, kwa kufuatana na shauri lako na la wengine wanaotii amri za Mungu. Yote yatendeke kwa kufuatana na Sheria.
Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.
Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kwa hiyo, nitawahukumu ninyi Waisraeli, kila mumoja wenu, kulingana na mwenendo wake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Mugeuke na kuachana na makosa yenu yasipate kuwaangamiza.
Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.
awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.