Ezra 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20027 Mufalme Kiro akawarudishia vyombo ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevitwaa kutoka katika nyumba ya Yawe na kuviweka katika nyumba ya miungu yake. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Vilevile akavirudisha vyombo vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevipeleka kutoka katika hekalu kule Yerusalema na kuviweka katika hekalu la Babeli. Vyombo hivyo Kiro akaviondoa toka hekalu la Babeli na kuvipatia Sesebasari ambaye alikuwa amemuchagua akuwe mutawala wa Yuda; akamwamuru akisema:
Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!