Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ezra 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mufalme Kiro akawarudishia vyombo ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevitwaa kutoka katika nyumba ya Yawe na kuviweka katika nyumba ya miungu yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ezra 1:7
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.


Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Nebukadneza akatwaa vilevile vyombo vimoja vya nyumba ya Yawe akavipeleka Babeli na kuviweka katika nyumba ya kifalme kule Babeli.


Vilevile akavirudisha vyombo vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevipeleka kutoka katika hekalu kule Yerusalema na kuviweka katika hekalu la Babeli. Vyombo hivyo Kiro akaviondoa toka hekalu la Babeli na kuvipatia Sesebasari ambaye alikuwa amemuchagua akuwe mutawala wa Yuda; akamwamuru akisema:


Vilevile, vyombo vyote vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alivileta Babeli kutoka katika hekalu la Yerusalema, vitarudishwa na kuwekwa kila kimoja pahali pake katika nyumba ya Mungu.”


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Bwana akamwacha Yoyakimu atiwe katika mikono ya mufalme Nebukadneza pamoja na sehemu ya vyombo vya nyumba ya Mungu. Basi mufalme Nebukadneza akakamata wafungwa na vyombo akavipeleka katika inchi ya Babeli, akaviweka katika hazina ya nyumba ya miungu yake.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ