Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mordekayi sasa akakuwa mutu mwenye madaraka makubwa katika nyumba ya kifalme, na habari zake zikaenea katika majimbo yote kwamba uwezo wake ulikuwa unazidi kuongezeka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:4
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.


Naye Daudi akazidi kuwa mukubwa kwa sababu Yawe wa majeshi alikuwa pamoja naye.


Daudi akakuwa na sifa popote katika inchi, naye Yawe akayatia hofu mataifa yote, nayo yakamwogopa sana.


Matendo yake yote makubwa na ya ajabu, pamoja na simulizi kamili juu ya jinsi alivyomupandisha Mordekayi cheo na kumupatia heshima kubwa, yote yameandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku cha ufalme wa Media na Persia.


Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.


Niliwatwanga, wakakuwa kama vumbi inayopeperushwa na upepo; niliwakanyaga kama matope katika barabara.


Watu wa haki wanastawi kama mingazi; wanakomaa kama mierezi ya Lebanoni!


Yawe akawafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri. Tena, Musa mwenyewe akakuwa mutu mukubwa sana katika inchi ya Misri na mbele ya wakubwa na mufalme na watu wote.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.


Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.


Basi, Yawe alikuwa pamoja na Yoshua na sifa zake zikaenea katika inchi yote.


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ