Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Halafu malkia Esteri, binti ya Abihaili, akaandika barua kwa mamlaka yake yote, pamoja na Mordekayi Muyuda kuhakikisha ile Mordekayi aliyoiandika pale mbele juu ya Purimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:29
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ukafika wa Esteri kwenda kwa mufalme. Huyo, binti wa marehemu Abihaili, binamu ya Mordekayi, na ambaye alilelewa na Mordekayi, hakuomba kitu chochote zaidi ya kile alichopangiwa na Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wa mufalme. Esteri akapata kukubaliwa mbele ya kila mutu aliyemwona.


Kwa amri ya mufalme, tangazo hili lilitolewa katika muji mukubwa wa Susani, nao wajumbe wakalitangaza katika majimbo yote. Mufalme na Hamani wakaikaa chini kwa kunywa wakati watu katika muji wa Susani wanafazaika.


Mordekayi alikuwa ameandika barua hizo kwa jina la mufalme Ahasuero, akazipiga muhuri kwa pete ya mufalme. Na waliozipeleka walikuwa wajumbe waliopanda juu ya farasi wenye nguvu wanaokimbia mbio.


Mordekayi aliandika mambo haya yote. Kisha akaandika barua kwa Wayuda wote waliokuwa katika utawala wa Ahasuero.


Aliwaonya kila mwaka washike sikukuu, siku ya kumi na ine na siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari.


Vilevile walikubaliana kwamba kila jamaa ya Kiyuda, kizazi kwa kizazi, katika kila jimbo na muji, sharti ikumbuke siku za Purimu na kuzisherehekea siku zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ