Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:27
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


Mordekayi aliandika mambo haya yote. Kisha akaandika barua kwa Wayuda wote waliokuwa katika utawala wa Ahasuero.


Aliwaonya kila mwaka washike sikukuu, siku ya kumi na ine na siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari.


Vilevile walikubaliana kwamba kila jamaa ya Kiyuda, kizazi kwa kizazi, katika kila jimbo na muji, sharti ikumbuke siku za Purimu na kuzisherehekea siku zote.


kusudi wamwekee Mungu tumaini lao, wasipate kusahau matendo ya Mungu, lakini washike amri zake,


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Mugeni anayenitambua mimi Yawe asifikiri hivi: Hakika Yawe atanitenga na watu wake. Naye towashi asiseme: Mimi ni muti wenye kukauka!


Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,


Nawe utakumbuka mienendo yako na kupata haya wakati nitakapokupa wadada zako, mukubwa na mudogo, kama wabinti zako, ingawa si kwa sababu ya agano kati yangu na wewe.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Katika vizazi vyote vinavyokuja, masharti yaleyale mutakayofuata ninyi ndiyo mugeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi atakayofuata; mbele ya Yawe mutakuwa sawa.


Hakufanya agano hilo na wazee wetu, lakini alilifanya na sisi wote ambao tuko wazima hivi leo.


Yoshua akafanya nao mapatano ya amani; akafanya agano kwamba atawaruhusu kuishi. Viongozi wa Waisraeli wakawaapia kutimiza mapatano hayo.


Kila mwaka wanawake wa Israeli wanaenda kuomboleza kwa siku ine kifo cha binti ya Yefuta wa Gileadi.


Tangu siku ile Daudi alifanya uamuzi ule kuwa sharti na agizo katika inchi ya Israeli mpaka hivi leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ