Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:25
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

tafazali wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kwa kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kwa kadiri ya haki yake.


Tena alipogundua kwamba Mordekayi alikuwa Muyuda, akaamua kwamba kumwazibu peke yake haitoshi. Basi akafanya shauri la kuwaangamiza Wayuda wote, watu wa ukoo wa Mordekayi, katika utawala wa mufalme Ahasuero.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”


Hapo mufalme Ahasuero akamwuliza malkia Esteri: “Ni nani huyo anayesubutu kufanya jambo kama hilo? Yuko wapi mutu huyo?”


Ee Yawe, Bwana wangu, mukombozi wangu mukubwa, umenikinga salama wakati wa vita.


Ee Yawe, usiwape waovu vitu wanavyotaka, wala mipango yao mibaya usiifanikishe.


Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe, wakati mimi ninaponyoka.


Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Uharibifu wake utamurudilia yeye mwenyewe; ukali wake utamwangukia yeye mwenyewe.


Atawarudishia uovu wao wenyewe, atawateketeza kwa sababu ya ubaya wao. Yawe, Mungu wetu, atawateketeza kabisa!


Anayechimbia mwenzake shimo, anatumbukia ndani mwenyewe; anayewaporomoshea wengine jiwe, litamurudilia mwenyewe.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Lakini siku moja, –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi– ule musumari uliopigiliwa pahali pagumu utaregea kwa uzito. Utakatwa na kuanguka. Yawe amesema.


Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.


Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ