Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:22
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.


Aliwaonya kila mwaka washike sikukuu, siku ya kumi na ine na siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari.


Basi, Wayuda wakakubaliana kufanya kama walivyoanza na kama vile Mordekayi alivyowaandikia.


Ee nafsi yangu, umusifu Yawe! Usisahau hata kidogo matendo mazuri yake yote.


wawalipize mataifa kisasi, wawaazibu watu;


Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”


Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha; umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.


Lakini panga zao wenyewe zitawapenya mioyo, na pinde zao zitavunjwavunjwa.


Ewe Israeli, wakati Yawe atakapokufariji nyuma ya mateso, mahangaiko na utumwa uliofanyiwa,


Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!


Basi muwasaidie wamasikini na vitu vya ndani, na vingine vyote vitakuwa safi kwenu.


Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.


“Kukiwa masikini wa jamaa yenu katika miji ya inchi ambayo Yawe atawapa, musikuwe wachoyo na wagumu kwake.


Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.


Kwa siku saba mutamufanyia Yawe, Mungu wenu, karamu pahali ambapo Yawe atachagua; kwa sababu Yawe, Mungu wenu atawabariki kwa mazao yenu yote na katika shuguli zenu zote nanyi hakika mutafurahi.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ