Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 9:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 9:19
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


Mordekayi aliandika mambo haya yote. Kisha akaandika barua kwa Wayuda wote waliokuwa katika utawala wa Ahasuero.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.


Basi muwasaidie wamasikini na vitu vya ndani, na vingine vyote vitakuwa safi kwenu.


“Kukiwa masikini wa jamaa yenu katika miji ya inchi ambayo Yawe atawapa, musikuwe wachoyo na wagumu kwake.


Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.


Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.


Miji yote hii ilikuwa na makimbilio yenye kuta ndefu zilizokuwa na milango na vifungio. Kulikuwa vilevile vijiji vingi ambavyo havikuzungukwa na kuta.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ