Halafu mufalme akamwambia malkia Esteri: “Katika muji mukubwa peke yake Wayuda wamewaua watu mia tano, pamoja na wana kumi wa Hamani. Unafikiri wamefanya nini kule katika majimbo! Unataka nini sasa? Maana utatimiziwa. Uniambie, unataka nini zaidi, nawe utapewa.”
Lakini Wayuda wa muji mukubwa wa Susani wakakusanyika vilevile siku ya kumi na ine lakini hawakupumzika. Walisherehekea siku ya kumi na tano kwa furaha na shangwe.