Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 “Ikikupendeza, ewe mufalme, na kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ukiona ni vizuri nami nikikupendeza, tafazali, toa tangazo la kuvunja mipango ambayo Hamani alikuwa ameamuru itimizwe. Mipango hiyo ni ile ya mwana wa Hamedata, wa uzao wa Agagi, aliyopanga kwa kuwaangamiza Wayuda wote katika majimbo yote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 8:5
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme akamupenda zaidi Esteri kuliko wanawake wote. Naye Esteri akapata kukubaliwa na kutendewa mema mbele yake zaidi kuliko wabinti wengine wote. Basi, mufalme akamuvalisha taji ya kimalkia kwenye kichwa, akamufanya malkia pahali pa Vashiti.


Yule atakayekupendeza zaidi, afanywe malkia pahali pa Vashiti.” Mufalme akaona shauri hilo ni jema, akafanya hivyo.


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Ahasuero akamupandisha Hamani cheo, akakuwa waziri mukubwa. Hamani alikuwa mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.


Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe mufalme, na ikikupendeza kukubali ombi langu, basi, ninaomba wewe na Hamani mukuje kesho kwenye karamu nyingine nitakayowaandalia. Wakati huo nitakujulisha ombi langu.”


Malkia Esteri akamujibu: “Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe mufalme, na ikikupendeza kunitimizia ombi langu, hitaji yangu ni mimi niishi na watu wangu vilevile.


Sasa basi, ninakusihi, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, unionyeshe sasa njia zako, kusudi nipate kukujua na kupata kukubaliwa mbele yako. Ninaomba ukumbuke vilevile kwamba taifa hili ni watu wako.


Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.


Aliniambia: ‘Uniruhusu niende kwa jamaa yangu, kwa maana wanatolea sadaka kule katika muji, na ndugu yangu amenitaka nikuwe pale. Hivyo kama nimepata kukubaliwa mbele yako, uniruhusu niende kwa wandugu zangu’. Ndiyo maana hayuko hapa kushiriki chakula cha mufalme.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ