Halafu, mufalme akavua pete yake ya muhuri kwenye kidole chake na kumuvalisha Yosefu. Akamuvalisha na nguo za kitani safi na mukufu wa zahabu kwa shingo.
Matendo yake yote makubwa na ya ajabu, pamoja na simulizi kamili juu ya jinsi alivyomupandisha Mordekayi cheo na kumupatia heshima kubwa, yote yameandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku cha ufalme wa Media na Persia.
Kisha Esteri akazungumuza tena na mufalme; akajitupa chini, kwenye miguu ya mufalme, naye akilia, akamusihi mufalme aukomeshe mupango mubaya ambao Hamani, wa uzao wa Agagi, alikuwa amepanga juu ya Wayuda.
Kisha mufalme Nebukadneza akamupandishia Danieli heshima kubwa, akamupa zawadi nyingi kubwakubwa, na kumufanya kuwa mutawala wa jimbo lote la Babeli, na mukubwa wa wenye hekima wote wa Babeli.
Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Mulete mbio kanzu nzuri sana na kumuvalisha nayo. Mumuvalishe pete kwenye kidole chake na mumuvalishe viatu.