Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 8:17
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo na wana wake walipokuwa wakisafiri, Mungu akawatia hofu wenyeji wa miji yote ya jirani hata hawakusubutu kuwafuatilia.


Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Siku hiyo ilikuwa ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari. Siku iliyofuata ya kumi na ine, wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na sherehe.


Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.


Katika kila muji wa kila jimbo wa mufalme Ahasuero, Wayuda walijitayarisha vizuri kumushambulia mutu yeyote ambaye angejaribu kuwazuru.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.


Nao viongozi wote wa majimbo, watawala, wakubwa na wakubwa wa mufalme vilevile waliwasaidia Wayuda, maana wote walimwogopa Mordekayi.


Wamisri walifurahia kuondoka kwao, maana hofu iliwashika kwa sababu yao.


Niliwatwanga, wakakuwa kama vumbi inayopeperushwa na upepo; niliwakanyaga kama matope katika barabara.


Kitisho na hofu vimewashika. Kwa sababu ya ukubwa wa nguvu zako, wao wamenyamaza kimya kama jiwe, mpaka watu wako, ee Yawe, wapite, mpaka watu wale uliowakomboa wamewapita.


Hakuna mutu yeyote atakayeweza kuwashambulia. Popote mutakapokwenda katika inchi hiyo, Yawe, Mungu wenu, atawatia watu hofu wawaogope, kama vile alivyowaahidi.


Leo nitaanza kuwafanya watu wote katika dunia wakuwe na woga na hofu juu yenu. Watasikia habari zenu nao watatetemeka na kufazaika.’


Mara tu tuliposikia mambo hayo, tukavunjika moyo kabisa kwa sababu yenu, tukaishiwa nguvu kabisa. Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia!


akawaambia: “Mimi ninajua kwamba Yawe amewapa inchi hii; tumepatwa na hofu juu yenu na wakaaji wote wa inchi hii wanatetemeka kwa sababu yenu.


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ