Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mordekayi alikuwa ameandika barua hizo kwa jina la mufalme Ahasuero, akazipiga muhuri kwa pete ya mufalme. Na waliozipeleka walikuwa wajumbe waliopanda juu ya farasi wenye nguvu wanaokimbia mbio.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 8:10
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yezebeli akaandika barua kwa jina la Ahabu na kuzipiga muhuri wa mufalme. Kisha akapeleka barua hizo kwa wazee na watu wenye heshima walioishi na Naboti kule katika muji.


Kwa hiyo wajumbe wakapita katika inchi yote ya Israeli na ya Yuda kwa kupeleka barua zile kufuatana na amri ya mufalme na wakubwa wake. Barua hizo zilikuwa na ujumbe huu: “Enyi watu wa Israeli muliobaki nyuma ya mashambulizi ya wafalme wa Asuria. Mumurudilie Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, kusudi naye apate kuwarudilia.


Munaweza kuwaandikia Wayuda neno lolote munalopenda. Tena munaweza kuandika kwa jina langu na kutumia muhuri wa kifalme, kwa sababu tangazo ambalo limetolewa kwa jina la mufalme na kupigwa muhuri wa mufalme, haliwezi kuvunjwa.”


Siku zangu zinaenda mbio kuliko mukimbiaji, zinakimbia bila kuona faida.


Amri ya mufalme ni shauri la mwisho. Nani anayesubutu kumwuliza: “Unafanya nini?”


Makundi ya ngamia yataifunika inchi yako, wana wa ngamia kutoka Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Seba. Watakuletea zahabu na ubani, wakitangaza sifa za Yawe.


Watawarudisha wandugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Yawe. Watawaleta juu ya farasi, juu ya nyumbu, juu ya ngamia na ndani ya magari na juu ya vipoyi mpaka Yerusalema, kwenye mulima wangu mutakatifu. Watawaleta kama Waisraeli wanavyoleta sadaka ya unga katika chombo safi mpaka ndani ya nyumba yangu mimi Yawe.


Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;


Ninakutumia kwa kuponda farasi na waaskari wapanda-farasi, magari ya kukokotwa na watembezaji wake.


Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi katika raha na amani katika nyumba yangu ya kifalme.


Sisi wakubwa uliotuweka, wasimamizi, maliwali, washauri na wakubwa wa majimbo, wote tumepatana kwamba inafaa, ee mufalme, utoe amri na kuhakikisha kwamba inafuatwa kikamilifu. Amuru kwamba kwa muda wa siku makumi tatu kusikuwe mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote kwa mungu yeyote au kwa mutu yeyote, isipokuwa kutoka kwako wewe, ewe mufalme. Mutu yeyote atakayevunja sheria hii atupwe katika pango la simba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ