Waadui zetu katika mataifa jirani, waliposikia kwamba kazi tumeimaliza, wakaogopa na kupata haya sana; maana walijua hakika kwamba kazi hii ilikamilika kwa musaada wa Mungu wetu.
Siku ileile, mufalme Ahasuero akamupatia malkia Esteri mali yote ya Hamani, adui ya Wayuda. Esteri akamujulisha mufalme kwamba Mordekayi ni ndugu yake. Basi, tangu wakati ule, Mordekayi akaruhusiwa kumwona mufalme.