Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 7:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 7:4
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini sisi ni sawa na Wayuda wengine; watoto wetu ni sawa na watoto wao. Hata hivyo, tunawalazimisha watoto wetu kuwa watumwa. Wabinti zetu wamoja wamekwisha kuwa watumwa. Hatuna uwezo wa kuzuia jambo hili maana mashamba yetu na mizabibu yetu inanyanganywa na watu wengine.”


Wajumbe wakazipeleka barua hizo kwa kila jimbo katika utawala ule. Tangazo hilo lilisema kwamba kwa siku moja tu, ni kusema siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari, Wayuda wote – tangia kwa vijana mpaka wazee, wanawake na watoto, wote wauawe, waangamizwe na kuteketezwa kabisa, na mali zao zote zinyanganywe.


“Ikikupendeza, ewe mufalme, amri itolewe, watu hawa waangamizwe. Nami ninaahidi, kama utaamuru hivyo, nitatoa kiasi cha kilo elfu kumi za feza iwekwe katika hazina ya mufalme.”


Hapo mufalme Ahasuero akamwuliza malkia Esteri: “Ni nani huyo anayesubutu kufanya jambo kama hilo? Yuko wapi mutu huyo?”


Esteri akamujibu: “Adui yetu mukubwa na mutesaji wetu, ni huyu mwovu Hamani!” Hapo Hamani akashikwa na hofu mbele ya malkia na mufalme.


Kwa njia ya barua hizi mufalme akawaruhusu Wayuda katika kila muji kukusanyika kwa kuyalinda maisha yao. Walikuwa na ruhusa ya kuharibu, kuua bila huruma na kuangamiza kundi lolote la watu au jimbo, lenye kuwashambulia kwa silaha pamoja na wanawake na watoto wao, na kunyanganya mali zao.


Maana, ninaweza namna gani kuvumilia kuona watu wangu wanaangamizwa na wandugu zangu wanauawa?”


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Mufalme Dario aliamua kuweka wakubwa mia moja na makumi mbili kwa kusimamia mambo ya ufalme.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao; na kuwauzisha wakosefu wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa.


Lakini kama mutumishi yule akijisemesha mwenyewe kwamba bwana wake anakawia kurudia; na halafu anaanza kuwapiga watumishi wenzake, wanaume na wanawake, naye anakula na kunywa na kulewa.


Yawe atawarudisha Misri kwa mashua, safari ambayo aliahidi kwamba hamungeifanya tena. Huko mutajaribu kujiuzisha kwa waadui zenu kuwa watumwa, lakini hakuna mutu atakayewanunua.”


Sasa, ninyi mumelaaniwa nanyi siku zote mutakuwa watumwa wa kukata kuni na kuchota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”


Wewe, ukae pamoja nami, wala usiogope. Maana, anayetafuta kuyaangamiza maisha yangu anatafuta hata yako vilevile. Ukiwa pamoja nami, uko salama kabisa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ