Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 7:10
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini yule mupishi mukubwa wa mikate akamutundika juu ya muti, kama vile Yosefu alivyokuwa amewaelezea ndoto zao.


Nyuma ya mambo yale, hasira yake ilipokwisha kutulia, mufalme Ahasuero akamukumbuka Vashiti, akakuwa anafikiri juu ya ugumu wake na hatua iliyokamatwa juu yake.


Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Mufalme akasimama kwa hasira, akatoka ndani ya chumba kwenye karamu ya divai na kwenda inje kwenye bustani ya nyumba ya kifalme. Hamani alipoona kwamba mufalme amekusudia kumwazibu, akabaki nyuma kwa kumusihi malkia Esteri ayaponyeshe maisha yake.


Kisha mufalme akarudi kutoka katika bustani, na mara alipoingia ndani ya chumba walimokuwa wanakunywa divai, akamukuta Hamani amejitupa karibu na kiti ambamo Esteri alikuwa ameikaa. Kuona hivyo, mufalme akasema kwa sauti kubwa: “Hivi mutu huyu anataka kumushika kwa nguvu malkia mbele yangu, tena ndani ya nyumba ya kifalme?” Mara tu mbele mufalme hajamaliza kusema, matowashi wakamufunika Hamani uso.


Mufalme Ahasuero akawaambia malkia Esteri na Mordekayi, yule Muyuda: “Muangalie! Nimemupa Esteri mali ya Hamani, naye wamekwisha kumutundika kwa sababu ya shauri lake baya juu ya Wayuda.


Mufalme akaamuru hayo yatimizwe, na tangazo likatolewa katika muji Susani. Wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya muti.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Miguu yake mwenyewe itamutia katika mutego; kila mara anatembea juu ya shimo.


Atatoweka kama ndoto, asionekane tena, atafutikana kama maono ya usiku.


Lakini panga zao wenyewe zitawapenya mioyo, na pinde zao zitavunjwavunjwa.


Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Atawarudishia uovu wao wenyewe, atawateketeza kwa sababu ya ubaya wao. Yawe, Mungu wetu, atawateketeza kabisa!


Anayetafuta kutenda mazuri anapata upendeleo, lakini anayetafuta kutenda maovu atapatwa na maovu.


Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.


Anayechimbia mwenzake shimo, anatumbukia ndani mwenyewe; anayewaporomoshea wengine jiwe, litamurudilia mwenyewe.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Ndivyo nitakavyomaliza hasira yangu, nami nitakuwa nimetuliza kasirani yangu na kufarijika ndani ya moyo. Hapo ndipo watakapojua kwamba mimi, Yawe, nimewaazibu kwa sababu ya wivu wangu kwa ukosefu wenu wa uaminifu.


Kwa hiyo mufalme akafurahi sana; akaamuru kwamba wamwondoe Danieli toka ndani ya pango. Basi wakamwondoa, naye hakuonekana na alama hata kidogo ya kidonda, kwa sababu alimutegemea Mungu wake.


Mufalme akaamuru wale watu waliomuchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake wao na watoto wao. Nao, hata mbele hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.


Kisha yule malaika aliyeongea nami akaniambia kwa sauti: Wale farasi waliokwenda katika inchi ya kaskazini wameituliza kasirani ya Yawe.


Samusoni akawaambia hao Wafilistini: “Kama hayo ndiyo muliyofanya, ninaapa kwamba sitaondoka mpaka nimelipiza kisasi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ